Shukran kwa kutkumbusha :-) 

> Date: Sun, 26 Jun 2011 16:03:57 +0300
> From: oslimoke@gmail.com
> To: wikimediake@lists.wikimedia.org
> Subject: [Wikimedia Kenya] Mwito wa Maelewano
>
> Kwa Wapenzi na Wapambe wa WMKE
> Wasaalam kutoka kwangu nikitarajia mpo vyema.Dhamira yangu ya kuandika
> barua hii ni kuwasii enyi wapenzi na wapambe wa WMKE tuwe na maelewano
> na kushirikiana katika shughuli zetu a kuendeleza ukuajia wa Wikipedia
> na usambazaji wa habari kwa wote
>
> ==Mizozo==
> Mara si haba nimetazama tukizomeana vikali(miye nkiwemo) katika nyuzi
> kadhaa a barua pepe.Swali langu ni kwa nini tuzomene ilhali sote
> tumejitolee kwa hiari kuandeleza usambai wa habari?pengine wengine
> wetu hatufahamu ni kwa nini tupo kwenye kundi hili le WMKE...hilo ndo
> jibu nimeng'amua kwa uchungu.kwa nini?ukitazama kwa umakini,nyuzi
> ziletazo udhia na tafash ni zile zilizo za kitu fulani,yaani
> "faida".utapata kila watu wachangia katika uzi huo sana.kinachokera
> sana ni tunapokuwa na uzi wa kung'amua na kuchangunua makala au miradi
> inayoohusu WMKE(kama vile Bylwas,WTN) nk,ni wachache sana hujitokea
> kuchangia kwa miradi hizi.Ilhali miradi hii haswa ndio maana ya kuwepo
> kwa WMKE na sio zile a "faida"
>
> ==kukosoana==
> Ni vyema kukosoana kila mara tunapoteleza.Miye nafurahi kukosolewa au
> mtu kukosoa mawazo au michango yangu.Lakini nadhani ingekuwa vyema
> tukosoane kwa heshima na pia toa suluhu au wazo mbadala,sio tu
> kunikosoa bila sababu.
>
> ==Heko==
> Mara nyingi tumesaha jinsi ya kuwapa na kutia watu motisha.Ningepende
> tusikosoane tu,bali kuwapongeza wenzetu na kuwapa heko kwa kazi nuri
> walo/wafanyazo.Hekow huwatia watu motisha wa kuendela kufanya
> vyema.Kwa hayo,miye binafsi ningependa kuwatia wafuata heko kwa kazi
> yao/michango yao katika kukua miradi na WMKE
>
> *Abbas-anashughulika maswala ya sheria(Bylaws) na pia anauunda
> wavuti(website) wetu kwa sasa...heko Abbas:-)
> *Alex-anashughulika mawsala ya WTN na pia yeye alitutengezea posta
> maridadi ya WikiSaturday ya JKUAT...kazi nzuri Alex
> *Steve-alisughulika na kuanda makala ya WikiSaturday ya JKUAT na pia
> ni mshrika mkuu.Alipiga chapa na kusambaza posta za WikiSaturday kwa
> kutumia hela ake...Heko Steve
>
> ...kama sijakutaja samahani,sijataka kuwahudhi watu na barua
> refu...sku nyingine na sijakusudia.
>
> Tafadhali:Nawaomba wanachama kutazama wavuti wa Wikipedia Takes
> Nairobi Hapa:http://en.wikipedia.org/wiki/Wikipedia:Wikipedia_takes_Nairobi/Goals
> na kuchangia ili tufanikishe mradi huu.
> Pia naomba wanachama watazame makala ya Abbas ya Sheria na kuyapiga
> msasa na kuchanganua kabla yatumwe kwani hizi ndizo sheria zitakazo
> tuongoa na ni vyuema kutoa mchango wako.
> Mwsiho tazama wavuti wetu hapa:
> http://wikimedia.or.ke/Visit_of_Asaf_Bartov_from_the_Wikimedia_Foundation
> ili tujadiliane kuhusu kuja kwa Asaf na vile twaweza kufaidi kwa ziara yake.
>
> p/s:nimetumia Swahili maana haya ni mambo yetu ya "ndani",..-)
> --
> Limoke Oscar,
>
> _______________________________________________
> WikimediaKE mailing list
> WikimediaKE@lists.wikimedia.org
> https://lists.wikimedia.org/mailman/listinfo/wikimediake